SERIKALI KUWAFUTA MACHOZI WADAU WA ZAO LA EMBE


Serikali imeahidi kuwasaidia Chama cha Wakulima wa Embe Nchini Amagro kupata huduma ya nishati ya Umeme katika vituo vyake vya ukusanyaji na usindikaji wa bidhaa za embe Wilayani Mkuranga.
Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Ludovick Nduhiye ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika Mkutano wa  Wadau wa Zao la Embe ambao umefanyika katika Uwanja wa Maonesho wa Mwl. J.K. Nyerere,barabara ya Kilwa Dar es Salaam.
Bw.Nduhiye amesema kuwa atahakisha anawasiliana na Taasisi zinazohusika na maswala ya nishati ya umeme ili waweze kupeleka nishati hiyo katika kituo hicho cha usindikaji wa embe Wilayani Mkuranga ambacho kimeombewa umeme kwa miaka minne mpaka hivi sasa hakijapata huduma hiyo kutokana na kuwa mbali na vyanzo vya umeme.
 Wakati wa Mkutano huo, Wadau wa Embe katika mnyororo wa thamani waliomba Serikari kuwasaidia miundombinu ya usafirishaji na uhufadhi wa embe, ambapo Naibu Katibu Mkuu ameahidi kuwasiliana na Wizara ya Kilimo ili waweze kupata ufumbuzi wa changamoto hiyo.
Mkutano huo umeratibiwa kwa ushirikiano wa Umoja wa Wakulima wa Zao la Embe (AMAGRO) pamoja na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade).

No comments

Powered by Blogger.